TAFAKARI: NAFSI KATIKA NENO
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
2 Timotheo 3:16
Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
Waebrania 4:12
Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Mwanzo 2:7
Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
Ufunuo wa Yohana 19:12-13
Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
Yohana 14:23
Bwana asifiwe watu wa Mungu. Tafakari uwezo na nguvu ndani ya neno.
1. *Lenye pumzi ya Mungu*
2. Li hai
3. Ni kali, lina choma, lina viungo na mafuta.
4. Linatambua mawazo na makusudi ya moyo.
--"akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai."
--"tutakuja kwake, na kufanya makao kwake."
Mbarikiwe sana na muwe na siku njema. MUNGU ANAWAPENDA.
Comments
Post a Comment