TAFAKARI: CHUMVI NA NURU
Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.
Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.
Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Mathayo 5:11,13,14,16
Bwana asifiwe watu wa Mungu. Chumvi na Nuru; kwa matendo yetu mema Baba yetu wa mbinguni atukuzwe. Mtashutumiwa, mtaudhiwa na mtanenewa mabaya kwa uongo, lakini mzidi katika kutenda mema.
Mbarikiwe sana na muwe na siku njema.
Comments
Post a Comment