Kama Mkristo uliyeokoka, ni lazima ujitambue wewe ni nani kwa sasa. Ni nini kilifanyika baada ya kumkubali Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako. Baada ya kuamini alifufuka kutoka wafu.
Haiwezekani una AK47, ukakimbizwa na mtu mwenye rungu. Tatizo kubwa watu wanamiliki silaha nzito lakini hawajijui. Mkristo unalogwa? Kwa nini? Mfano mkutano wa injili unazuiwa na wachawi, sio kweli.
Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda;
hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.
Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu;
Waefeso 2:4-6
Nini kimefanyika sasa baada ya hayo, na kwa nini tuna nguvu ya ajabu katika ulimwengu wa Roho.
aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;
juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
Waefeso 1:20-21
HIVYO KAMA MKRISTO JITAMBUE, JIAMINI. TAMBUA MAMLAKA ULIYO NAYO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, ILI UWEZE KUISHI VYEMA KATIKA ULIMWENGU HUU WA MWILI. Amina.
KWA KUONGEZA ZAIDI SOMA,
WAKOLOSAI 3:1-10
Comments
Post a Comment