TAFAKARI: WAKIWATUKANA
Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.
Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana.
1 Petro 4:1-4
Bwana asifiwe watu wa Mungu. Tujivike silaha ya nia ile ile, tukiishi katika mapenzi ya Mungu muda uliobaki hapa duniani. Maisha ya kutenda mapenzi ya Mataifa, kuenenda katika njia potofu, imetosha. Watawatukana, ila msiogope.
Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa.
Lakini mwisho wa mambo yote umekaribia; basi, iweni na akili, mkeshe katika sala.
1 Petro 4:5,7
Comments
Post a Comment