JE, KRISTO ALISEMA NINI KWENYE MFANO WA NGANO NA MAGUGU?
Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing'oa ngano pamoja nayo.
Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.
Mathayo 13:29-30
Upendo, Neema, Rehema na Amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu ziwe pamoja nanyi. Katika mfano huu, Kristo alisema viachwe vyote vikue ( ngano na magugu) mpaka siku ya mavuno ( mwisho wa dunia), ndipo malaika zake watachambua na kukusanya magugu na kuyachoma moto. Mwenye masikio na asikie.
Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.
Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,
na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio, na asikie.
Mathayo 13:40-43
Hivyo, ni vizuri tuzidi kujiandaa sababu hatujui hiyo siku wala hiyo saa, tukubali kuwa mbegu njema ambayo imepandwa na Mwana wa Adamu (ngano) na siyo magugu iliyopandwa na yule adui ibilisi.
Comments
Post a Comment