MPENDE MUNGU KWA KUMJUA KRISTO.
Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
Mathayo 22:38
Upendo na amani ya Mungu katika Kristo iwe pamoja nanyi. Namna mojawapo ya kumpenda Mungu ni kwa kumjua sana Kristo Yesu.
Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;
ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake;
Wafilipi 3:8,10
Hivyo, namna mojawapo ya kumpenda Mungu zaidi ni kwa kumjua sana Kristo Yesu. Na kwa ajili yake tuyahesabu kuwa hasara yale yaliyokuwa faida kwetu.
Comments
Post a Comment