BWANA ANAWAITAJE WACHUNGAJI WA UWONGO, NA WANGAPI WATAWAFUATA?
Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.
Mathayo 15:14
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Jina la Mungu linatukanwa kwa ajili yao, sababu wanayajua mapenzi ya Mungu, wanayakubali yaliyo bora, na wanajua wanaongoza vipofu. Ni wanafiki, maana wanaacha mambo muhimu yawapasayo kufanya, wanawaongoza vipofu kumbe na wao ni vipofu, wanatumbukia wote shimoni.
Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia.
Mathayo 23:24
Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa.
2 Petro 2:2
Comments
Post a Comment