NI NINI HUSABABISHA WAACHANE NA ZIZI LAO WENYEWE?
Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote.
Isaya 56:11
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Hawawezi kufahamu neno sababu wamegeuka upande wakifuata njia zao wenyewe kwa faida zao wenyewe. Wanatimiza mapenzi yao wenyewe badala kutimiza mapenzi ya Mungu. Ni walinzi vipofu wasio na maarifa, hawawezi kulia, huota ndoto, hulala na hupenda usingizi. Kipofu akimuongoza kipofu wanatumbukia shimoni wote wawili.
Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung'aa ya asubuhi.
Ufunuo wa Yohana 22:15-16
Comments
Post a Comment