VITU VINGINE VYA THAMANI ALIVYOAHIDIWA MSHINDI. (2)
Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kwa aliye na sikio asikie maneno haya ambayo Roho anayaambia makanisa.
YEYE ASHINDAYE:
1. Atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake.
Ufunuo wa Yohana 3:5
2. Nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.
Ufunuo wa Yohana 3:12
3. Nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
Ufunuo wa Yohana 3:21
Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.
Yakobo 1:12
Hivyo, tustahimili majaribu maana hayana budi kuja ili tukubaliwe na kuipokea taji ya uzima, pamoja na ahadi zingine zote tulizoahidiwa kama washindi.
Comments
Post a Comment