JE, MAANDIKO YANA UWEZO WA KUKUFANYIA NINI?
na ya kuwa tangu utoto umeyajua maandiko matakatifu, ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu kwa imani iliyo katika Kristo Yesu.
2 Timotheo 3:15
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.
Ili mtu wa Mungu awe kamili na apate kutenda matendo mema, kila andiko lenye pumzi ya Mungu lafaa kwa kufundisha, kumuonya mtu makosa yake, kumuongoza na kumuadabisha katika haki. Watu hawana neno la Mungu likakaa ndani yao, kwa sababu hawamwamini yule aliyetumwa na yeye.
Mwamini yule aliyetumwa (Kristo Yesu) ndipo uyachunguze maandiko.
Bali wewe ukae katika mambo yale uliyofundishwa na kuhakikishwa, kwa maana unajua ni akina nani ambao ulijifunza kwao;
2 Timotheo 3:14
lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
2 Timotheo 3:13
Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
Zaburi 119:99
Comments
Post a Comment