JE, MTUME PAULO ALILINGANISHA KANISA NA NINI?
Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake.
1 Wakorintho 12:27
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.
Mungu ameweka wengi katika kanisa na kila mmoja na karama yake. Viungo ni vingi ila mwili ni mmoja. Kiungo kimoja kikiumia vyote vimeumia nacho, na kimoja kikitukuzwa vyote hufurahi pamoja nacho. Hivyo, kanisa tu viungo vya mwili wake Kristo.
Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;
Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.
Warumi 12:4-5
Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.
Waefeso 5:29
Comments
Post a Comment