JE, NENO LA MUNGU LINASEMA NINI KUHUSU WALIOIJUA NJIA NA HAWATEMBEI NDANI YAKE?
Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
2 Petro 2:21
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Neno linasema kuijua kweli na njia ya haki, na kuiacha na kurudi na kuendelea ni sawasawa na mbwa aliyerudia matapiko yake na nguruwe aliyeoshwa na kurudi kugaa-gaa matopeni. Unatakiwa kuijua kweli, na hiyo kweli ikuweke huru kweli kweli. Unatakiwa uijue kwa kupata maarifa ili usiangamizwe. Maana watu wa Mungu wanaangamizwa na sacbabu kubwa ni kukosa maarifa, na maarifa utayapata kwa kulisikiliza Neno La Mungu moyoni mwako.
Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.
Yuda 1:4
Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
Mithali 18:15
Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi.
Luka 12:47-48
Comments
Post a Comment