KATIKA KUSAMEHE, NI MFANO GANI TUUFUATE?
Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,
mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
Wakolosai 3:12-13
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tukiwasamehe watu makosa yao, na Baba yetu wa mbinguni atatusamehe makosa yetu, tukichukuliana kwa upendo.
tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
Waefeso 4:32
kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;
Waefeso 4:2
Comments
Post a Comment