NI, JAMBO GANI KRISTO ALILOOMBA KWA BABA KWA NIABA YA WANAFUNZI WAKE?
Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.
Yohana 17:11
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Jambo kuu umoja wao ulilo nao ni UPENDO. Na amri mpya aliyotupa Bwana wetu Yesu Kristo ni tupendane sisi kwa sisi, na tuwe na umoja kama wao walivyo na umoja wenye upendo wa ajabu sana.
Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu.
Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Yohana 17:15-21
Comments
Post a Comment