JE, TUNAWEZA KUJUA SIKU NA SAA YA KUJA KWAKE MWANA WA ADAMU?
Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.
Mathayo 24:36
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.
Kwa habari ya kuja kwake Mwana wa Adamu, ni Baba peke yake aijuae siku ile na saa ile. Inafananishwa na siku za Nuhu; ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu, watu hawakutambua, ikaja Gharika ikawachukua wote. Watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa. Kesheni maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana.
Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
1 Wathesalonike 5:1-2
Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.
Mathayo 24:44
Comments
Post a Comment