JE, YESU ALIWAAMBIA WANAFUNZI KUWA ULE MWISHO ULIKUWA KARIBU WAKATI HUO?
Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
Mathayo 24:6
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.
Yesu aliwaambia waangalie mtu asiwadanganye, maana wengi watakuja na watadanganya kwa jina lake. Mengi yatatokea lakini ule mwisho bado. Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali. Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu.
Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.
Mathayo 24:5
Mimi nimekuja kwa jina la Baba yangu, wala ninyi hamnipokei; mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea huyo.
Yohana 5:43
Comments
Post a Comment