KWA NINI NI MUNGU MWENYE WIVU?
Maana hutamwabudu mungu mwingine, kwa kuwa Bwana, ambaye jina lake ni mwenye wivu, ni Mungu mwenye wivu.
Kutoka 34:14
Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;
Wakolosai 3:5
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.
Wivu wa Mungu unasababishwa na wewe kutokutenda mapenzi yake, yaani kutokutenda yaliyo mema. Maana maovu ni sawa tu na kuabudu sanamu, na imeandikwa tusiabudu miungu mingine ila yeye tuu Yehova, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tusiwe vuguvugu; kama baridi kuwa baridi, na kama moto kuwa moto.
Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, nawapatiliza wana uovu wa baba zao; hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
Kumbukumbu la Torati 5:9
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.
Wagalatia 5:19-21
Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.
Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?
1 Wakorintho 10:21-22
Comments
Post a Comment