NI KWA NJIA GANI KILA ANDIKO LILITOLEWA NA KWA KUSUDI GANI?
Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;
ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
2 Timotheo 3:16-17
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.
Ili mtu wa Mungu awe kamili na apate kutenda matendo mema, kila andiko lenye pumzi ya Mungu lamfaa kumfundisha, kumuonya makosa yake, kumuongoza na kumuadabisha katika haki. Mtu wa Mungu uyakimbie mabaya, ukafuate haki, utauwa, imani, upendo, saburi, upole. Tuwafundishe watu kuyakubali maneno yenye uzima ya Bwana wetu Yesu Kristo, mafundisho yapatanayo na utauwa.
Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.
Warumi 15:4
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
2 Petro 1:21
Comments
Post a Comment