JE, BAADA YA KUTUBU MTU ANAPASWA KUISHIJE?
Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi?
Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?
Warumi 6:1-2
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake, tulizikwa pamoja naye kwa nia ya huo ubatizo ili kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, na sisi tuenende katika upya wa uzima. Utu wetu wa kale ulisulubishwa pamoja naye, ili miili yetu ya dhambi ibatilike, tusitumikie dhambi tena. Hivyo, tujihesabu kuwa wafu kwa dhambi, na tulio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu. Na dhambi isitawale ndani ya miili yetu ipatikanayo na mauti, hata tukazitii tamaa zake, tujitoe kwa Mungu kama walio hai baada ya kufa.
Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema.
Warumi 6:14
Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
1 Petro 4:2
Comments
Post a Comment