JE, KRISTO ALISEMA ALIKUJA ULIMWENGUNI KUFANYA NINI?
Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu.
Waebrania 10:7
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Alisema alikuja ili ayafanye mapenzi yake, Mungu. Maana sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi, Mungu hakupendezwa nazo. Haikuwezekana damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi, sababu katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka; dhabihu hazingekoma kutolewa. Mungu alimuwekea Yesu Kristo mwili tayari, ili tupate utakaso kwa mwili huo mara moja tu. Kwa ajili ya dhambi dhabihu hiyo moja ni idumuyo milele.
Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.
Waebrania 10:14,18
Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.
Zaburi 40:6,8
Comments
Post a Comment