JE, NI KWA UHAKIKA GANI KRISTO ALIWAKEMEA MAFARISAYO?
Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?
Mathayo 15:3
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Aliwaambia kwamba wanalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yao. Aliwaita wanafiki, akisema ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zao, kuwa wanamheshimu Mungu kwa midomo, ila mioyo yao iko mbali na Mungu. Na wanamwabudu Mungu bure, wakifundishana mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Akasema hao ni viongozi vipofu wa vipofu.
Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walicho nacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa;
Isaya 29:13
Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Wakolosai 2:23
Comments
Post a Comment