JE, TOBA INAPASWA KUHUBIRIWA KWA NANI, NA NI NANI WALIOITWA KUTUBU?
na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.
Luka 24:47
Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi, wapate kutubu.
Luka 5:32
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Wenye afya hawahitaji kutibiwa, isipokuwa walio hawawezi. Kwa jina la Yesu, habari ya toba na ondoleo la dhambi itahubiriwa mataifa yote sababu alikuja kuwaita wenye dhambi wapate kutubu na sio wenye haki.
Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.
Luka 15:7
akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli;
2 Timotheo 2:25
Comments
Post a Comment