LINAPOTUMIKA KATIKA UNABII, NENO KUTIMILIZA LINAMAANISHA NINI?
Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.
Mathayo 5:17
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Neno kutimiliza lilitumika:
1. Kumaanisha kutimia au kutokea kwa jambo lililosemwa na manabii na torati.
ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,
Mathayo 4:14
Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda.
1 Wakorintho 15:54
2. Kufanya, au kutenda kulingana, (kuhusishwa na wajibu).
Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali.
Mathayo 3:15
Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema.
Yakobo 2:8
Comments
Post a Comment