AINA MBILI ZA TAFAKARI.
1. MAWAZO MEMA. (NENO LA MUNGU).
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Zaburi 119:11
2. MAWAZO MABAYA. (YA YULE MWOVU).
Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
Mithali 6:18
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Ukitafakari vema na mawazo mema utatenda mema, bali ukitafakari vibaya na mawazo mabaya utatenda maovu. Tafakari na mawazo yako ndio matendo yako yatakavyokuwa, na matendo yako yanapelekea kuwa tabia yako. Kutafakari neno la Mungu inakupelekea kutenda mema na kunakuepusha kutenda dhambi, lakini unavyotafakari na kuwa na mawazo mabaya inakupelekea kutenda dhambi. Tuangushe mawazo na kila kijiinucho juu ya elimu ya Mungu kwa neno la Mungu maana silaha za vita vyetu si za mwili na zina uwezo katika Mungu wa kuangusha ngome na kuteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.
Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
Yoshua 1:8
Comments
Post a Comment