JE, WATU WA MUNGU WANAITWAJE SASA, NA WALIKUWAJE KABLA YA KUTEULIWA?
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.
1 Petro 2:9-10
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Wafumbuliwe macho yao, wageuke waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za shetani nakumwelekea Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwa Kristo Yesu. Mungu alisema, Nuru itang'aa toka gizani mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo. Kwa maana zamani tulikuwa giza, sasa tumekuwa nuru katika Bwana, hivyo tuenende kama watoto wa nuru, tupate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka na kati yao mwaonekana kama mianga katika ulimwengu.
Ni kama vile alivyosema katika Hosea, Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu, Na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu.
Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, Ninyi si watu wangu, Hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai.
Warumi 9:25-26
Comments
Post a Comment