HALAFU MWILI WA MTU HUWA NINI?
Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
1 Wakorintho 6:19
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Tumekuwa hekalu la Mungu, na Roho wa Mungu anakaa ndani yetu. Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo, sababu hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo sisi. Maana tulinunuliwa kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani ya Kristo Yesu , hivyo tumtukuze Mungu katika miili yetu.
Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu.
1 Wakorintho 7:23
Comments
Post a Comment