JE, AHADI ZA MUNGU ZIMEWEKWA ULIMWENGUNI KWA SABABU GANI?
Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.
2 Petro 1:4
Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Ni ili tupate kuwa washarika wa tabia za Uungu, tukiokolewa na uharibifu uliomo humu duniani unaosababishwa na tamaa. Ametukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tujitahidi sana kwa upande wetu, katika imani yetu tutie na wema, katika wema wetu maarifa, katika maarifa yetu kiasi, katika kiasi chetu saburi, katika saburi yetu utauwa, katika utauwa wetu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, UPENDO.
Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
1 Petro 2:9
mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,
Wafilipi 2:15
Comments
Post a Comment