JE, IMANI PEKE YAKE ITAMWOKOA MTU?
Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
Mtu akisema anayo imani, aonyeshe imani yake kwa njia ya matendo yake; maana isipokuwa na matendo imekufa nafsini mwake. Mtu anaamini ya kuwa Mungu ni mmoja, atenda vema, ila na mashetani nao wanaamini na kutetemeka.
Ibrahimu alihesabiwa kuwa ana haki kwa matendo alipomtoa mwanawe juu ya madhabahu, na hapa tunaona kwamba imani ilitenda kazi pamoja na matendo yake, ya kwamba imani ile ilikanilishwa kwa njia ya matendo yale.
Mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake. Mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.
Si kila amwambiaye Kristo Yesu, Bwana , Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni, ila yeye afanyaye mapenzi ya Mungu Baba yetu aliye mbinguni.
Yakobo 2:14-26, Mathayo 7:21.
Comments
Post a Comment