JE, WAMWAMINIJE YEYE WASIYEMSIKIA?
Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu.
Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema!
Lakini si wote walioitii ile habari njema. Kwa maana Isaya asema, Bwana, ni nani aliyeziamini habari zetu? Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako, na ni lile neno la imani tulihubirilo.
Hivyo basi, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na ukaamini moyoni mwako ya kuwa Mungu Baba yetu wa Mbinguni alimfufua katika wafu utaokoka. Maana kwa moyo mtu huamini na kupata haki, na kwa kinywa mtu hukiri na kupata wokovu.
Sasa basi kumwamini Kristo Yesu usiyemsikia huja kwa kusoma neno la Kristo ambalo ni neno la Mungu Baba yetu, na kutoka kwa wahubirio habari ya mema. Kwa maana hatujihubiri wenyewe, bali Kristo Yesu ya kuwa ni Bwana na sisi wenyewe kuwa tu watumishi wenu kwa ajili ya Yesu. Kwa kuwa maneno aliyopewa Kristo Yesu alitupa kupitia wanafunzi wake, nao wakayapokea na wakajua hakika kuwa ametoka kwa Baba yetu mbinguni na kusadiki kwamba yeye ndiye aliyemtuma.
Warumi 10, 2 Wakorintho 4:5,
Yohana 17:8
Comments
Post a Comment