Skip to main content

KUJUA SIRI YA MUNGU.

KUJUA SIRI YA MUNGU.

    NEEMA NA IWE KWENU, NA AMANI, ZITOKAZO KWA MUNGU BABA YETU.
    TUFARIJIKE MIOYO YETU, TUKIUNGANISHWA KATIKA UPENDO, TUPATE UTAJIRI WOTE WAKUFAHAMU KWA HAKIKA, NA TUPATE KUJUA SIRI YA MUNGU, YAANI NDANI YA KRISTO HAZINA ZOTE ZA HEKIMA NA MAARIFA ZIMESITIRIKA.
    MTU ASIJE KUWADANGANYA  KWA MANENO YA KUWASHAWISHI.
    KRISTO AKAE MIOYONI MWETU KWA IMANI TUKIWA NA SHINA NA MSINGI KATIKA UPENDO; ILI TUPATE KUFAHAMU PAMOJA NA WATAKATIFU WOTE JINSI ULIVYO UPANA, NA UREFU NA KIMO NA KINA, NA KUUJUA UPENDO WAKE KRISTO, UPITAO UFAHAMU KWA JINSI ULIVYO MWINGI, TUPATE KUTIMILIKA KWA UTIMILIFU WOTE WA MUNGU.
    MWENYE MWILI AWAYE YOTE ASIJE AKAJISIFU MBELE ZA MUNGU, BALI KWA YEYE TUMEKUWA KATIKA KRISTO YESU, ALIYEFANYWA HEKIMA ITOKAYO KWA MUNGU, NA HAKI, NA UTAKATIFU, NA UKOMBOZI, ILI KAMA ILIVYOANDIKWA, YEYE AONAYE FAHARI NA AONE FAHARI JUU YA BWANA.
    SIRI ILE ILIYOFICHWA TANGU ZAMANI ZOTE NA TANGU VIZAZI VYOTE, BALI SASA IMEFUNULIWA KWA WATAKATIFU WOTE.
    TUSIENENDE KAMA MATAIFA WAENENDAVYO, KATIKA UBATILI WA NIA ZAO, SABABU AKILI ZAO ZIMETIWA GIZA, NAO WAMEFARAKANISHWA NA UZIMA WA MUNGU SABABU YA UJINGA NDANI YAO NA UGUMU WA MIOYO YAO.
MKAVAE UTU MPYA, ULIOUMBWA KWA NAMNA YA MUNGU KATIKA HAKI NA UTAKATIFU WA KWELI.

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...