MCHUNGAJI WANGU MWEMA .
1. BWANA NDIYE MCHUNGAJI WANGU, SITAPUNGUKIWA NA KITU:
Bwana wetu Yesu Kristo ndiye mchungaji mwema; maana mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake; humwona mbwa mwitu anakuja, huwakimbia na kuwaacha kondoo, na mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya. Tulio wake Kristo Yesu anatujua, na tulio wake tunamjua, kama Baba amjuavyo yeye, na yeye amjuavyo Baba, na ameutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Kristo Yesu, alitukanwa, aliteswa, akajikabidhi kwake ahukumuye kwa haki. Akazichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili tuwe wafu kwa mambo ya dhambi, na tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake tumepona. Tulikuwa tunapotea kama kondoo, lakini sasa tumemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zetu. Mchungaji mwema huacha wale kondoo tisii na kenda na kwenda kumtafuta yule mmoja aliyepotea, maana ni furaha mbinguni kwa mmoja mwenye dhambi atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda wasio na haja ya kutubu.
Wenye afya hawahitaji tabibu bali walio hawawezi. Mchungaji mwema, Bwana wetu Yesu Kristo hakuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.
Zaburi 23:1, Yohana 10:11, 1 Petro 2:25, Luka 15:4, Luka 5:30
Comments
Post a Comment