Skip to main content

MCHUNGAJI WANGU MWEMA

MCHUNGAJI WANGU MWEMA .

1. BWANA NDIYE MCHUNGAJI WANGU, SITAPUNGUKIWA NA KITU:
  Bwana wetu Yesu Kristo ndiye mchungaji mwema; maana mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake; humwona mbwa mwitu anakuja, huwakimbia na kuwaacha kondoo, na mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya. Tulio wake Kristo Yesu anatujua, na tulio wake tunamjua, kama Baba amjuavyo yeye, na yeye amjuavyo Baba, na ameutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
    Kristo Yesu, alitukanwa, aliteswa, akajikabidhi kwake ahukumuye kwa haki. Akazichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili tuwe wafu kwa mambo ya dhambi, na tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake tumepona. Tulikuwa tunapotea kama kondoo, lakini sasa tumemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zetu. Mchungaji mwema huacha wale kondoo tisii na kenda na kwenda kumtafuta yule mmoja aliyepotea, maana ni furaha mbinguni kwa mmoja mwenye dhambi atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda wasio na haja ya kutubu.
   Wenye afya hawahitaji tabibu bali walio hawawezi. Mchungaji mwema, Bwana wetu Yesu Kristo hakuwaita wenye haki, bali wenye dhambi wapate kutubu.

Zaburi 23:1, Yohana 10:11, 1 Petro 2:25, Luka 15:4, Luka 5:30

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...