Skip to main content

MPINGA KRISTO YUAJA, NA WENGI WAMEKUWEPO.

MPINGA KRISTO YUAJA, NA WENGI WAMEKUWEPO.

Neema na amani na ziongezwe kwetu.
    Ni wakati wa mwisho, na kama mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja; sio hivyo tuu hata wakati huo walikuwepo. Tumepakwa mafuta na yeye akiye mtakatifu, hivyo tunajua yote. Hatukuandikiwa sisi kwa sababu hatujui iliyo kweli, bali kwa sababu tunaijua, tena hakuna uongo wo wote utokao katika hiyo kweli. Aliye mwongo ni yule akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo; na huyu ndiye mpinga Kristo, amkanaye Baba na Mwana. Basi tulilosikia tangu mwanzo likikaa ndani yetu nasi tutakaa ndani ya Mwana,  na ndani ya Baba.
    Kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu, na hii ndio roho ya mpinga Kristo ambayo tumesikia yaja, na sasa tayari imekwisha kuwako duniani. Hivyo tusiamini kila roho, bali tuzijaribu hizo roho kama zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. Twamjua Roho wa Mungu, na kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu.
    Tujihadhari na manabii wa uongo, watu waliovalia mavazi ya kondoo kumbe ndani ni mbwa-mwiti wakali. Tusimzimishe Roho wala tusitweze unabii, bali tujaribu mambo yote kwa kulishika lililo jema na kwa kujitenga na ubaya wa kila. Ukimjua Mungu, utumjua Roho wa kweli na roho ya upotevu.

1 Yohana 2:18-22,24, 1 Yohana 4:3,1,2,
Mathayo 7:15

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...