Skip to main content

MTAKUWA WATAKATIFU KWA KUWA YEYE NI MTAKATIFU.

MTAKUWA WATAKATIFU KWA KUWA YEYE NI MTAKATIFU.

Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
    Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki, maana ufalme wa mbinguni ni wao. Tujapoteswa kwa sababu ya haki tuna heri. Tusiogope kutisha kwao wala tusifadhaike , bali tumtakase Kristo Bwana mioyoni mwetu. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake husikiliza maombi yao. Hakuna wa kutudhuru, tukiwa wenye juhudi katika mema. Tukistahimili tutendapo matendo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.
    Tumjibu kila mtu habari za tumaini lililo ndani yetu, kwa upole na kwa hofu. Tuwe na dhamiri njema, ili lile neno tunalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wetu mwema katika Kristo. Tuwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili kwa kutusingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yetu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
    Mungu Baba yetu, kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu. Tuwe na kiasi, tukiitumainia kwa utimilifu ile neema katika ufunuo wa Yesu Kristo; kama watoto wa kutii tusijifananishe na taama za kwanza za ujinga wetu, bali kama yeye alivyo mtakatifu, nasi tuwe watakatifu katika mienendo yetu yote; kwa maana imeandikwa, tutakuwa watakatifu kwa kuwa yeye ni mtakatifu.

Mathayo 5:10, 1 Petro 3:12-16,
1 Petro 2:20,12, 1 Petro 1:3,13-16.

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...