Skip to main content

TU WARITHI KWA MUNGU PAMOJA NA KRISTO.

TU WARITHI KWA MUNGU PAMOJA NA KRISTO.

Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
    Roho wa Mungu anakaa ndani yetu, hivyo hatuufuati mwili, bali tunaifuata roho. Na wote tunaoongozwa na Roho wa Mungu, ndio wana wa Mungu. Hatukupokea tena roho ya utumwa iletayo hofu, bali roho ya kufanywa wana, na kwa hiyo twalia Aba, yaani Baba. Roho  mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kuwa sisi tuu watoto wa Mungu; hivyo kama watoto, tu warithi wa Mungu, turithio pamoja na Kristo, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
    Basi sisi si watumwa tena bali tu wana,  na kama wana tu warithi kwa Mungu. Tulikuwa chini ya sheria, tukakombolewa ili tupate hali ya kuwa wana; na kwa kuwa tumekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye Aba, yaani, Baba. Na kama sisi ni wa Kristo, tumekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
    Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi. Mungu, ametufanya imara katika Kristo, katutia mafuta na ametutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu. Basi tufahamu sana haya yasemwayo, maana Bwana atatupa akili katika mambo yote.

Warumi 8:17(9,14-17), Wagalatia 4:7,5,6,
Wagalatia 3:29, 2 Timotheo 1:7,
2 Wakorintho 1:21-22, 2 Timotheo 2:7.

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...