TUACHANE NA UTOTO, ILI KUUKULIA WOKOVU.
Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
Tukiangalia maandiko, tunaona kuna kuzaliwa kiroho na kuna ukuaji. Na ukuaji kiroho inaonyesha kabisa ni kwa ulaji wa neno la Mungu. Hivyo basi kama watoto wachanga tuliozaliwa sasa tuyatamani maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo tupate kuukulia wokovu, ikiwa tumeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.
Ukuaji wa kiroho unapaswa kukamilika kufikia ukomavu wa kiroho. Tunahuburi habari za Kristo, tukimwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu katika hekima yote kumleta kila mtu mtimilifu katika Kristo.
Kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo, kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu na huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe. Na tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, mtu awe mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo. Tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila za watu, kwa ujanja, tukifuata njia za udanganyifu. Tushike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, yaani Kristo Yesu.
1 Petro 2:2-3, Wakolosai 1:28,
Waefeso 4:7-15
Comments
Post a Comment