TUKAE NDANI YAKE, NA YEYE NDANI YETU.
Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
Katika mfano Kristo Yesu alioutumia hapa, anatuambia yeye ndiye mzabibu wa kweli, na Mungu Baba yetu ndiye mkulima. Na kila tawi ndani yake lizaalo, hulisafisha lizidi kuzaa, bali tawi lisilozaa huliondoa. Sisi tumekwisha kuwa safi kwa neno lake. Hivyo, tukae ndani yake, na yeye ndani yetu.
Yeye ni mzabibu; sisi ni matawi; tukaao ndani yake naye ndani yetu, twazaa sana maana pasipo yeye sisi hatuwezi kufanya neno lo lote. Tukikaa ndani yake na maneno yake yakikaa ndani yetu, tuombe tutakalo lote nasi tutatendewa.
Kama vile mwili ni mmoja, una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo. Kiungo kimoja kikiumia, vyote huumia nacho, au kimoja kikitukuzwa, vyote hufurahi pamoja nacho. Basi tumekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke.
Yohana 15:1-7, 1 Wakorintho 12:12,26,27.
Comments
Post a Comment