Skip to main content

UMOJA TULIOITIWA ILI TURITHI BARAKA.

UMOJA TULIOITIWA ILI TURITHI BARAKA.

Neema na amani na ziongezwe kwetu.
    Tuwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu; watu tusiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo tuliyoitiwa ili turithi baraka. Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila, Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana.
    Tuwabariki wanaotuudhi; tubariki, wala tusilaani. Tufurahi pamoja nao wafurahio; tulie pamoja nao waliao. Tupatane nia zetu sisi kwa sisi. Tusinie yaliyo makuu, lakini tukubali kushughulishwa na mambo manyonge. Tusiwe watu wa kujivunia akili. Tusimlipe mtu ovu kwa ovu. Tuangalie yaliyo mema machoni pa watu wote. Tukae katika amani na watu wote. Tusijilipize kisasi, bali tuipishe ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.
    Maneno yetu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu. Tumesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino; Lakini Kristo anatuambia, tusishindane na mtu mwovu; lakini mtu atupigaye shavu la kuume, tumgeuzie na la pili. Atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia. Atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili. Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo. Kristo pia anatuambia, tuwapende adui zetu, tuwaombee wanaotuudhi, ili tupate kuwa wana wa Baba yetu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
    Maana tukiwapenda wanaotupenda sisi twapata thawabu gani? Tena tukiwaamkia ndugu zetu tu, tunatenda tendo gani la ziada? Hata watoza ushuru na watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? Tuwaonye wale wasiokaa kwa utaratibu; tuwatie moyo walio dhaifu; tuwatie nguvu wanyonge; tuwavumilie watu wote. Mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote tulifuate lililo jema, sisi kwa sisi na kwa watu wote. Kristo Yesu alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.
    Ni nani atakayetudhuru, tukiwa wenye juhudi katika mema? Tusishindwe na ubaya, bali tuushinde ubaya kwa wema. Basi hapo tutakuwa wakamilifu, kama Baba yetu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

1 Petro 3:8-11,13, Warumi 12:14-19,21, Mathayo 5:37-48,
1 Wathesalonike 5:14-15, 1 Petro 2:23.

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...