VINAVYOONEKANA NI VYA MUDA. VISIVYOONEKANA NI VYA MILELE.
Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
Ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. Na Mungu, Baba yetu wa mbinguni atujalie kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, tufanywe imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho wake, katika utu wa ndani.
Dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; Hivyo basi, tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele. Tuyahesabu mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Kwa imani twajua ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.
2 Wakorintho 4:16-18, Waefeso 3:16, Warumi 8:18, Waebrania 11:1,3
Comments
Post a Comment