WAPANDAO WALA WATIAO MAJI SI KITU, BALI AKUZAYE. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo. Apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. Hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu? Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa ...
KARIBU KWENYE BLOG YENYE TAFAKARI NA MASOMO YA NENO LA MUNGU. MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI; NDIVYO MEMA YATAKAVYOJIA. NENO LAKE ULIWEKE MOYONI MWAKO.