Skip to main content

HATUJAPEWA ROHO YA WOGA.

HATUJAPEWA ROHO YA WOGA.

Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu katika Kristo Yesu.
    Tuzichochee karama za Mungu zilizo ndani yetu, maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu, na ya upendo na ya moyo wa kiasi. Hivyo tusiuonee haya ushuhuda wa Bwana wetu, bali tuvumilie mabaya kwa ajili ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu. Mungu alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa matendo yetu sisi bali kwa makusudi yake yeye na neema yake tuliyopewa katika Kristo Yesu tangu milele.
     Tunaoongozwa na Roho wa Mungu, ndio wana wa Mungu na hatukupokea tena roho ya utumwa iletayo hofu, bali tulipokea roho ya kufanywa wana. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu kuwa sisi tu watoto wa Mungu, na tu warithi wa Mungu turithio pamoja na Kristo, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Tumepewa msaidizi, Roho Mtakatifu, ambaye Baba ametupa kwa jina la Kristo Yesu, atufundishe yote, atukumbushe yote ambayo Kristo alituambia. Ndipo Kristo Yesu akatuambia; Amani ametuachia, amani yake ametupa, na alivyotupa yeye sivyo kama ulimwengu utoavyo. Hivyo tusifadhaike mioyoni mwetu, wala tusiwe na woga.

1 Timotheo 1:6-10, Warumi 8:14-17,
Yohana 14:26-27.

Comments

Popular posts from this blog

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU.

MAWAZO YA MUNGU NA NJIA ZAKE SI MAWAZO YETU WALA NJIA ZETU. Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.     Mawazo yake si mawazo yetu, wala njia zetu si njia zake; kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zake zi juu sana kuliko njia zetu, na mawazo yake kuliko mawazo yetu, asema BWANA. Hivyo tumtafute BWANA, maadamu anapatikana, na tumwite, maadamu yu karibu. Mtu mbaya na uache njia yako, na usiye haki uache mawazo yako, umrudie BWANA naye atakurehemu, urejee kwa Mungu wetu, naye atakusamehe kabisa. Anayajua mawazo anayokuwazia wewe, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kukupa wewe tumaini siku zako za mwisho.   Nawe utamwita, utaenda na kumuomba, naye atakusikiliza; utamtafuta, na kumuona, utakapomtafuta kwa moyo wako wote.     BWANA asema hivi, Niite, name nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Na itakuwa kila atakayeliitia jina la B...