JE! DANIELI ALISEMA NINI KUHUSU
UFALME WA MUNGU?
Neema na iwe kwetu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na
kwa Bwana Yesu Kristo.
Ufalme na mamlaka,
na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye
juu; ufalme wake ni wa milele, na watu wote wenye mamlaka watamtumikia na
kumtii. Aliona katika njozi za usiku, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja
pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu
naye. Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na
taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele,
ambayo haitapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.
Malaika akamwambia
Mariamu, usiogope, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Utachukua mimba na kuzaa
mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana
wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.
Ufalme wa dunia utakuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki
hata milele na milele.
DANIELI 7:27,13,14, LUKA 1:30-33, UFUNUO WA YOHANA 11:15.
Comments
Post a Comment