Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2019

NI NANI PEKEE ANAWEZA KUWA MSHINDI?

NI NANI PEKEE ANAWEZA KUWA MSHINDI? Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu? 1 Yohana 5:5 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu. 1 Yohana 3:9 Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; nawe ujizoeze kupata utauwa. Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye. 1 Timotheo 4:7-8 Hivyo, kupata ushindi, amini kwamba  Yesu ni Mwana wa Mungu na ndiye Kristo, na usitende dhambi. Kama umezaliwa na Mungu, jizoeze kupata utauwa sababu ya uzima wa sasa na wa baadae. Amani,  Upendo, Neema na Rehema za Mungu zidumu pamoja nanyi.

NI JINSI GANI PETRO ALITHIBITISHA MAHUBIRI YAKE YA UJIO WA KRISTO?

NI JINSI GANI PETRO ALITHIBITISHA MAHUBIRI YAKE YA UJIO WA KRISTO? Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. 2 Petro 1:16 Neema na rehema za Mungu ziwe pamoja nanyi. Petro hapa anatuthibishia kwamba maneno haya ya kinabii sio kwamba ameyasikia kwa mtu bali alikuwa na Bwana wetu Yesu Kristo, aliona ukuu wake na alisikia sauti kutoka mbinguni kwa Mungu baba ikisema " huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, niliyeridhishwa naye" walipokuwa naye. Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu. Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing'aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. 2 Petro 1:18-2...

JE, NI AHADI GANI ALIYOPEWA MSHINDI?

JE, NI AHADI GANI ALIYOPEWA MSHINDI? Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure. Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:4,6,7 Neema na rehema za Mungu zowe pamoja nanyi. Kwa makwazo na mateso mbalimbali utakayokutana nayo hapa ulimwenguni, usiogope, kuwa na saburi maana kuna ahadi uliyopewa na Mungu utakapoweza kuyashinda yote. Utakuwa mwana na utarithi vyote, na wala hakutakuwa kwako na taabu tena. Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema. Warumi 12:21 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya k...

NI JINSI GANI MAUTI ILIKUJA ULIMWENGUNI?

NI JINSI GANI MAUTI ILIKUJA ULIMWENGUNI? Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; Warumi 5:12 Amani na Upendo wa Mungu zidumu pamoja nanyi. Ni kwa ajili ya mtu mmoja, dhambi ilikuja ulimwenguni kwa watu wote. Na kwa dhambi hiyo mauti ikawafikia watu wote. Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. Warumi 6:23 Hivyo, mauti ilikuja kwa kutokutii na kutenda dhambi kwa mtu mmoja..

NI MUHIMU KULA KILA KILICHO HALALI PEKEE?

NI MUHIMU KULA KILA KILICHO HALALI PEKEE? Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo. 1 Wakorintho 10:23 Bila shaka hapa Paulo anazungumzia vitu tunavyoweza kula. Anasema kwa Mkristo kwa kufahamu, akila chakula ambacho ni sadaka kwa sanamu, naye atakuwa mshiriki wa ibada hiyo. Ila asipojua akila sio shida. Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri. Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri. Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu. 1 Wakorintho 10:27,28,31 Hivyo, shida ni pale unapojua ni chakula kwa ajili ya sadaka. Bora kutoulizauliza  kwa ajili ya dhamiri.

UKWELI NI KUUISHI SIO KUJIFUNZA TUU.

UKWELI NI KUUISHI SIO KUJIFUNZA TUU. Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi. Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako. Zaburi 119:11-12 Upendo na amani ya Mungu katika Kristo iwe pamoja nanyi. Ukweli ni kuuishi huo ukweli, sio tuu kuusikia na kujifunza katika Neno kwa kuhubiriwa habari njema. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia. Basi, kwa kuwa neno hili limebaki kwamba wako watu watakaoingia humo, na wale waliohubiriwa habari ile zamani walikosa kuingia kwa sababu ya kuasi kwao, Waebrania 4:2,6 Walakini mimi, hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka 1 Samweli 12:23 Hivyo, tuliishi neno sio kulisikia na kujifunza tu peke yake, tusitende dhambi.

MPENDE MUNGU KWA KUMJUA KRISTO.

MPENDE MUNGU KWA KUMJUA KRISTO. Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Mathayo 22:38 Upendo na amani ya Mungu katika Kristo iwe pamoja nanyi. Namna mojawapo ya kumpenda Mungu ni kwa kumjua sana Kristo Yesu. Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; Wafilipi 3:8,10 Hivyo, namna mojawapo ya kumpenda Mungu zaidi ni kwa kumjua sana Kristo Yesu. Na kwa ajili yake tuyahesabu kuwa hasara yale yaliyokuwa faida kwetu.

UNABII KWENYE MAANDIKO SIO TAFSIRI BINAFSI.

UNABII KWENYE MAANDIKO SIO TAFSIRI BINAFSI. Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing'aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. 2 Petro 1:19-21 Neema na Rehema zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu ziwe pamoja nanyi. Unabii sio kutafsiri apendavyo mtu, bali ni kunena yaliyotoka kwa Mungu. Tujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo ya maana. Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu, 2 Timotheo 2:16 Hivyo, tujiepushe na mambo yasiyo ya maana, yasiyo ya dini, maana unabii mwingi wa sasa ni wa kunena mapenzi ya wanadamu.

WATASEMA NINI WALIO GIZANI KUHUSU UJIO WA BWANA?

WATASEMA NINI WALIO GIZANI KUHUSU UJIO WA BWANA? Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe, na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa. 2 Petro 3:3-4 Neema na Rehema zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu ziwe pamoja nanyi. Ni jambo la kawaida sana kusikia watu wakiuliza, " alisema atarudi, mbona harudi?" Tena wakidhihaki " Nisubiri mpaka lini, mpaka Yesu arudi?" Bila kufahamu kwamba hata wakati wa gharika ilikuwa hivyo hivyo, dunia ikaangamia kwa maji, ila kwa sasa ni kwa moto. Ni upendo tuu, ndio maana anakawia. Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 2 Petro 3:9 Hivyo, ni vizuri tuzidi kujiandaa sababu hatujui hiyo siku wala hiyo saa, maana kuja lazima...

MAISHA BINAFSI YA IBADA

MAISHA BINAFSI YA IBADA. Tunahitaji sana kuwa na maisha binafsi ya ibada, ili kuwa karibu zaidi na Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo. Maisha binafsi ya ibada yanahitaji mambo makuu matatu: 1. Muda wa utulivu. 2. Mahali tulivu. 3. Moyo wa utulivu. Ibrahimu akatoka asubuhi kwenda mahali aliposimama mbele za Bwana, Mwanzo 19:27 Yakobo akaondoka asubuhi na mapema, akalitwaa lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo, na kumimina mafuta juu yake. Mwanzo 28:18 Nawe uwe tayari asubuhi, na asubuhi ukwee juu katika mlima wa Sinai, nawe hudhurisha nafsi yako kwangu huko katika kilele cha mlima. Kutoka 34:2 Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko.  [YESU] Marko 1:35 Hivyo ni muhimu sana kuwa na maisha binafsi ya ibada ile uweze kufanikiwa kuwa karibu zaidi na Mungu.

TUKESHE NA KUWA NA KIASI

TUKESHE NA KUWA NA KIASI Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. 1 Wathesalonike 5:1-2 Neema na Rehema za Mungu ziwe pamoja nanyi. Kwa habariya ile siku hakuna haja ya kuandikiwa maana twafahamu yaja kama mwivi. Ulishapata kuwa wa nuru na mwana wa mchana wala si wa giza na usiku, ile siku haitakupata kama mwivi. Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi. Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza. Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi. 1 Wathesalonike 5:4-6 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru, kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; Waefeso 5:8-9 Hivyo, ni vizuri tuzidi kujiandaa sababu hatujui hiyo siku wala hiyo saa, na tukeshe ( kuwa na maisha binafsi ya ibada )...

JE, KRISTO ALISEMA NINI KWENYE MFANO WA NGANO NA MAGUGU?

JE, KRISTO ALISEMA NINI KWENYE MFANO WA NGANO NA MAGUGU? Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing'oa ngano pamoja nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu. Mathayo 13:29-30 Upendo, Neema, Rehema na Amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu ziwe pamoja nanyi. Katika mfano huu, Kristo alisema viachwe vyote vikue ( ngano na magugu) mpaka siku ya mavuno ( mwisho wa dunia), ndipo malaika zake watachambua na kukusanya magugu na kuyachoma moto. Mwenye masikio na asikie. Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia. Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi, na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa B...

NI MAMBO GANI YATAKAYOJITOKEZA ZAIDI NYAKATI ZA MWISHO?

NI MAMBO GANI YATAKAYOJITOKEZA ZAIDI NYAKATI ZA MWISHO? Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao. 2 Timotheo 3:1-5 Upendo, Neema, Rehema na Amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu ziwe pamoja nanyi. Nyakati za mwisho ni nyakati hatari sana sababu watu watakosa upendo, na hatutapendana sisi kwa sisi. Bali watu watapenda na kuthamini zaidi mali na fedha kuliko utu na utii. Watu watapenda starehe kuliko Mungu tena mbaya zaidi wakijifanya watakatifu. Na sio kwamba maovu yatapungua, yatazidi kuongezeka. lakini watu wabaya na wadangan...

UJIO WA KRISTO UMEFANANISHWA NA WAKATI GANI?

UJIO WA KRISTO UMEFANANISHWA NA WAKATI GANI? Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Mathayo 24:37 Upendo, Neema, Rehema na Amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu ziwe pamoja nanyi. Ujio wa Kristo umelinganishwa na siku za Nuhu. Hakuna mtu aijuaye, wala malaika wala Mwana, ni Baba peke yake. Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake. Mathayo 24:36 Tunachotakiwa ni kujiuliza ni nini kilitokea siku zile za Nuhu, na watu walikuwa katika mazingira gani? Je, walikuwa wanafahamu? Je, walikuwa wamejiandaa? Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. Mwanzo 6:5-6 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nu...

KWA NINI KUOMBA NA KUSHUKURU?

KWA NINI KUOMBA NA KUSHUKURU? Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Wafilipi 4:6 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema na faraja. Kuomba na kushukuru, ni kuonyesha uaminifu na ni mapenzi ya Mungu kwetu katika Kristo. Tukeshe tukiomba anamaanisha tusichoke kuomba, ila tuu tusiache kushukuru. Kuomba na kushukuru ndicho kinachokuweka karibu na Bwana, maana kushukuru kunaonyesha UAMINIFU. Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani; Wakolosai 4:2 Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu. Zaburi 145:18 Hivyo basi, tusijisumbue kwa neno lolote bali tudumu katika kusali na kuomba, bila kusahau kushukuru, maana Bwana yu karibu tukimwita kwa UAMINIFU.

ENENDA KAMA YEYE ALIVYOENENDA.

ENENDA KAMA YEYE ALIVYOENENDA. Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda. 1 Yohana 2:6 Amani na Upendo wa Mungu uwe pamoja nanyi. Kwa Mkristo kuwa mkamilifu, inampasa kuishi namna Kristo alivyoishi. Kikubwa ni Upendo maana ndio kifungo cha ukamilifu na ndiyo amri mpya aliyotupa, tupendane. Upendo utakuweka mbali na dhambi, na kuwa mkamilifu katika Kristo. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu. Wakolosai 3:14 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Yohana 13:34 Hivyo basi tuwe na Upendo kama Kristo alivyotupenda na tuwatendee wengine mema kama yeye alivyotutendea.

MOYO HUAMINI NA KINYWA HUKIRI.

MOYO HUAMINI NA KINYWA HUKIRI. Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Warumi 10:9-10 MAANA YEYE NI BWANA WA WOTE. Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. Warumi 10:12-13 WAMSIKIEJE PASIPO MHUBIRI? Basi wamwiteje yeye wasiyemwamini? Tena wamwaminije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikieje pasipo mhubiri? Tena wahubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri kama nini miguu yao wahubirio habari ya mema! Warumi 10:14-15 SI WOTE WALIOITII. Lakini si wote walioitii ile habari njema. Kwa maana Isaya asema, Bwana, ni nani aliyeziamini habari zetu? Warumi 10:16

MKIYAFISHA MATENDO YA MWILI KWA ROHO

MKIYAFISHA MATENDO YA MWILI KWA ROHO: Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili, kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:12-17

SIKU ZETU KAMA UA LA KONDENI

SIKU ZETU KAMA UA LA KONDENI Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo. Maana upepo hupita juu yake, kumbe haliko! Na mahali pake hapatalijua tena. Zaburi 103:15-16 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake. Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake. 1 Petro 2:21-22

UTULIVU NA MUNGU

UTULIVU NA MUNGU. Muda wako binafsi wa utulivu na Mungu, kunaongeza mahusiano na Mungu na ndio chanzo cha nguvu. Mfano wa muda binafsi na Mungu tunauona kwa Yesu mwenyewe, alikuwa akitoka na kwenda pasipo na watu kuomba. Hata alfajiri na mapema sana akaondoka, akatoka akaenda zake mahali pasipokuwa na watu, akaomba huko. Marko 1:35 Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye. Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni. Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba, Luka 22:39-41 Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba. Luka 5:16 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. Mathayo 6:6

MWAYACHUNGUZA MAANDIKO

MWAYACHUNGUZA MAANDIKO Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima. Yohana 5:39-40 Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona. Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye. Yohana 5:37-38

AKAWAHURUMIA, AKAWAPONYA.

AKAWAHURUMIA, AKAWAPONYA. Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao. Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao. Mathayo 14:13-14 Amani na Upendo wa Mungu uwe pamoja nanyi. Yesu ni mwenye huruma na anaponya bila kujali wewe ni mwenye haki au sio. Hata hivi leo wagonjwa wanapona kwa huruma yake, ila kwa kinachohitajika ni imani. Amina.

AMEPEWA MAMLAKA YOTE

AMEPEWA MAMLAKA YOTE Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. Mathayo 28:18-20 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Marko 16:15-16

SIKU ZA MWISHO. NYAKATI HATARI

SIKU ZA MWISHO. NYAKATI ZA HATARI Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake; hao nao ujiepushe nao. 2 Timotheo 3:1-5

TUNDA LA ROHO

TUNDA LA ROHO Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Wagalatia 5:16,22-25

FANYENI YOTE KWA SHUKRANI

FANYENI YOTE KWA SHUKRANI Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani. Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye. Wakolosai 3:15,17

MNA UZIMA WA MILELE

MNA UZIMA WA MILELE Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima. Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu. 1 Yohana 5:10-13

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO

TU WARITHI PAMOJA NA KRISTO Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye. Warumi 8:16-17 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu. Wagalatia 4:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu. Ufunuo wa Yohana 21:7

WASINGALIKUWA NA DHAMBI.

WASINGALIKUWA NA DHAMBI. Kama nisingalikuja na kusema nao, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao. Yeye anichukiaye mimi humchukia na Baba yangu. Kama nisingalitenda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa wametuona mimi na Baba yangu, na kutuchukia. Yohana 15:21-24

KAZI YA MUNGU

KAZI YA MUNGU Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye. Yohana 6:29 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo. Ufunuo wa Yohana 22:12 Kazi ya Mungu ni kumwamini aliyetumwa. Na huyohuyo aliyetumwa ndiye mlipaji. Kazi kweli kweli, utalipwa kwa kazi yako ilivyo. Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina.