Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2020

JE, TUNAPASWA KUTUBU KWA NANI, NA KUONYESHA IMANI KWA NANI?

JE, TUNAPASWA KUTUBU KWA NANI, NA KUONYESHA IMANI KWA NANI? nikiwashuhudia Wayahudi na Wayunani wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo. Matendo ya Mitume 20:21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Baada ya Yesu kutoka nyikani alikoongozwa na Roho, akiwako huko siku arobaini, hali akijaribiwa na shetani, alikokuwa pamoja na wanyama wa mwitu na malaika wakiwa wanamhudumia; alienda Galilaya akihubiri Habari Njema ya ufalme wa Mungu akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili. Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia. Mathayo 4:17 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana; Matendo ya Mitume 3:19 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kris...

JE, NI NAMNA GANI TUNATAKASWA TUTOKE KATIKA DHAMBI?

JE, NI NAMNA GANI TUNATAKASWA TUTOKE KATIKA DHAMBI? bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. 1 Yohana 1:7 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Kwa damu yake Kristo Yesu ambaye kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itasafisha dhamiri zetu na matendo maovu tupate kumwabudu Mungu. Hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu, tumepata utakaso. tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake, Ufunuo wa Yohana 1:5 Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa...

JE, NI AHADI GANI ILITOLEWA KWA WALE WANAOKIRI DHAMBI ZAO?

JE, NI AHADI GANI ILIYOTOLEWA KWA WALE WANAOKIRI DHAMBI ZAO? Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. 1 Yohana 1:9 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Tukisema kwamba hatuna dhambi au kwamba hatukutenda dhambi  twajidanganya wenyewe na kumfanya Mungu mwongo, wala kweli haimo mwetu na neno lake halimo mwetu. Yeye ni mwema sana na mwaminifu sana na wa haki. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema. Mithali 28:13

JE, MUNGU ANAMWANGALIA MTU WA NAMNA GANI?

JE, MUNGU ANAMWANGALIA MTU WA NAMNA GANI? Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu. Isaya 66:2 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Mbingu ni kiti chake cha enzi, na nchi(dunia) ni pa kuwekea miguu yake. Je, ni nyumba gani mtakayomjengea, au ni mahali gani atakapostarehe, si kwa mkono wake uliofanya haya yote? asema Bwana. Hakai katika nyumba zilizofanywa kwa mikono. Bwana yu katika hekalu lake takatifu, ambapo kiti chake kiko mbinguni. Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa. Zaburi 34:18 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau. Zaburi 51:17

JE, AFANYAYE DHAMBI NI MTUMWA WA NANI?

JE, AFANYAYE DHAMBI NI MTUMWA WA NANI? atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. 1 Yohana 3:8 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Atendaye dhambi afanya uasi, maana dhambi ni uasi. Yesu alidhihirishwa ili aziondoe dhambi na kuzivunja kazi za ibilisi, na dhambi haimo ndani yake. Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi. Ibilisi alikuwa mwuaji tangu mwanzo, wala hakusimama katika kweli. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe, sababu yeye pia ni muongo na baba wa huo, na hamna hiyo kweli ndani yake. Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi. 1 Yohana 5:18

JE, BAADA YA KUTUBU MTU ANAPASWA KUISHIJE?

JE, BAADA YA KUTUBU MTU ANAPASWA KUISHIJE? Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Warumi 6:1-2 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake, tulizikwa pamoja naye kwa nia ya huo ubatizo ili kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, na sisi tuenende katika upya wa uzima. Utu wetu wa kale ulisulubishwa pamoja naye, ili miili yetu ya dhambi ibatilike, tusitumikie dhambi tena. Hivyo, tujihesabu kuwa wafu kwa dhambi, na tulio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu. Na dhambi isitawale ndani ya miili yetu ipatikanayo na mauti, hata tukazitii tamaa zake, tujitoe kwa Mungu kama walio hai baada ya kufa. Kwa maana dhambi haitawatawala ninyi, kwa sababu hamwi chini ya sheria, bali chini ya neema. Warumi 6:14 Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika m...

JE, TOBA YA KWELI INAHUSISHA NINI?

JE, TOBA YA KWELI INAHUSISHA NINI? Tupilieni mbali nanyi makosa yenu yote mliyoyakosa; jifanyieni moyo mpya na roho mpya; mbona mnataka kufa, enyi nyumba ya Israeli? Ezekieli 18:31 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Ukirudi, ukaghairi, na kuyaacha makosa yako yote, uovu wako hautakuwa uharibifu kwako. Msienende tena kama Mataifa waenendavyo, ambao akili zao zimetiwa giza, wamefarakanishwa na uzima wa Mungu, sababu ya ujinga ndani yao na ugumu wa mioyo yao. Mvue mwenendo wa kwanza utu wa zamani kwa kufuata tamaa zenye kudanganya na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu. mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli. Waefeso 4:24

JE, TOBA INAPASWA KUHUBIRIWA KWA NANI, NA NI NANI WALIOITWA KUTUBU?

JE, TOBA INAPASWA KUHUBIRIWA KWA NANI, NA NI NANI WALIOITWA KUTUBU? na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Luka 24:47 Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi, wapate kutubu. Luka 5:32 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Wenye afya hawahitaji kutibiwa, isipokuwa walio hawawezi. Kwa jina la Yesu, habari ya toba na ondoleo la dhambi itahubiriwa mataifa yote sababu alikuja kuwaita wenye dhambi wapate kutubu na sio wenye haki. Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu. Luka 15:7 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; 2 Timotheo 2:25

JE, NI KWA UHAKIKA GANI KRISTO ALIWAKEMEA MAFARISAYO?

JE, NI KWA UHAKIKA GANI KRISTO ALIWAKEMEA MAFARISAYO? Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? Mathayo 15:3 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Aliwaambia kwamba wanalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yao. Aliwaita wanafiki, akisema ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zao, kuwa wanamheshimu Mungu kwa midomo, ila mioyo yao iko mbali na Mungu. Na wanamwabudu Mungu bure, wakifundishana mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu. Akasema hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walicho nacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa; Isaya 29:13 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili. Wakolosai 2:...

JE, MWOKOZI ALISEMA NINI KUHUSU KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU?

JE, MWOKOZI ALISEMA NINI KUHUSU KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU? Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Mathayo 7:21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Alisema tuihadhari na manabii wa uongo, watu wanaotujia wamevaa mavazi ya kodoo, kumbe ni mbwa mwitu. Mtawatambua kwa matunda yao, maana mti mwema huzaa matunda mazuri, na mti mwovu hazaa matunda mabaya. Tuyafanye mapenzi ya Baba yetu wa mbinguni hapa duniani. Mtu anatakiwa kuwa na imani yenye matendo mema (mapenzi ya Mungu). Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. Yakobo 1:22 Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa? Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. Yakobo 2:14,26

JE, KRISTO ALISEMA ALIKUJA ULIMWENGUNI KUFANYA NINI?

JE, KRISTO ALISEMA ALIKUJA ULIMWENGUNI KUFANYA NINI? Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu. Waebrania 10:7 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Alisema alikuja ili ayafanye mapenzi yake, Mungu. Maana  sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi, Mungu hakupendezwa nazo. Haikuwezekana damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi, sababu katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka; dhabihu hazingekoma kutolewa. Mungu alimuwekea Yesu Kristo mwili tayari, ili tupate utakaso kwa mwili huo mara moja tu. Kwa ajili ya dhambi dhabihu hiyo moja ni idumuyo milele. Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa. Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi. Waebrania 10:14,18 Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka. Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo f...

LINAPOTUMIKA KATIKA UNABII, NENO KUTIMILIZA LINAMAANISHA NINI?

LINAPOTUMIKA KATIKA UNABII, NENO KUTIMILIZA LINAMAANISHA NINI? Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Mathayo 5:17 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Neno kutimiliza lilitumika:  1. Kumaanisha kutimia au kutokea kwa jambo lililosemwa na manabii na torati. ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mathayo 4:14 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda. 1 Wakorintho 15:54 2. Kufanya, au kutenda kulingana, (kuhusishwa na wajibu). Yesu akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali. Mathayo 3:15 Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema. Yakobo 2:8

WAAAMINI HAWA UTAISHI.

WAAAMINI HAWA UTAISHI. Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Yohana 14:1 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi. Luka 10:28 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. TUMUAMINI MUNGU, BABA YETU ALIYE MBINGUNI. TUMUAMINI YULE (KRISTO YESU) ALIYETUMWA NA YEYE (MUNGU). TUMUAMINI ROHO MTAKATIFU, AMBAYE KRISTO ALITUOMBEA KWA BABA ATUPE AWE MSAIDIZI WETU YEYE ALIPOONDOKA. Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye. Yohana 6:29 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. Yohana 14:16-17 Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Yohana 14:12

JE, ILIKUWA KUSUDI LA KRISTO KUMALIZA AU KIBADILISHA SEHEMU YOYOTE YA SHERIA YA MUNGU?

JE, ILIKUWA KUSUDI LA KRISTO KUMALIZA AU KIBADILISHA SEHEMU YOYOTE YA SHERIA YA MUNGU? Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. Mathayo 5:18 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Yesu hakuja kuitangua torati na manabii, bali kutimiliza. Ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itenguke nukta moja ya torati. Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe. Luka 21:33 Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka. Waebrania 8:13 Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. Warumi 10:4

MWOKOZI WETU ALIMWAMBIA NINI YULE MTU ALIYETAKA WOKOVU?

MWOKOZI WETU ALIMWAMBIA NINI YULE  MTU ALIYETAKA WOKOVU? Akamwambia, Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Mathayo 19:17 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Mtu huyu alimuuliza Yesu, atende jambo gani jema ili apate uzima wa milele? Ndipo akamjibu, azishike amri, maana aliye mwema ni mmoja, naye ni Mungu. Na pia akitaka kuwa mkamilifu, aende akauze alivyo navyo, atoe sadaka(awape maskini), naye atakuwa na hazina yake mbinguni. Kwa kuwa hazina yako ilipo, ndipo utakapokuwapo na moyo wako. Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako. Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi. Luka 10:27-28

NI NINI TABIA YA SHERIA YA MUNGU?

NI NINI TABIA YA SHERIA YA MUNGU? Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. Warumi 7:14 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Torati si dhambi, na tusingalitambua dhambi ila kwa sheria; mfano tusingejua kutamani, kama torati isingalisema , Usitamani. Kuyajua mapenzi ya Mungu, na kuyakubali mambo yaliyo bora, umeelimishwa katika torati. Tazama, mimi naliumbwa katika hali ya uovu; Mama yangu alinichukua mimba hatiani. Zaburi 51:5 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho. Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili. Yohana 3:6-7

NI NINI TABIA YA MATENDO YA MUNGU?

NI NINI TABIA YA MATENDO YA MUNGU? Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu, Maagizo yake yote ni amini, Yamethibitika milele na milele, Yamefanywa katika kweli na adili. Zaburi 111:7-8 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Sheria ya Bwana kamilifu, huiburudisha nafsi. Ushuhuda wake ni amini, humtia mjinga hekima. Maagizo yake ni ya adili, huufurahisha moyo. Amri yake ni safi, huyatia macho nuru. Hukumu zake ni kweli, zina haki kabisa. Zinaonya; na kuzishika kuna thawabu nyingi. Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa. Ufunuo wa Yohana 15:3-4

JE, NI NINI KINACHOSEMWA JUU YA UTHABITI WA TABIA YA MUNGU?

JE, NI NINI KINACHOSEMWA JUU YA UTHABITI WA TABIA YA MUNGU? Kwa kuwa mimi, Bwana, sina kigeugeu; ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo. Malaki 3:6 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Hana kigeugeu (habadiliki). Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifanya kuwa zuri? Kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka. Karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake. Hukumu zake hazichunguziki, wala njia zake hazitafutikani. Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. Maombolezo 3:22 Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake. 1 Yohana 1:5

JE, KUNA WATOA SHERIA WANGAPI?

JE, KUNA WATOA SHERIA WANGAPI? Mtoa sheria na mwenye kuhukumu ni mmoja tu, ndiye awezaye kuokoa na kuangamiza. U nani wewe umhukumuye mtu mwingine? Yakobo 4:12 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi. Basi tusihukumu maana mtoa sheria na mwenye hukumu ni mmoja. Ndugu tusisingiziane au kuhukumuiana ndugu. Pia hatujui yatakayokuwa kesho, maana yeye anaweza kuokoa na kuangamiza. Kwa hiyo, wewe mtu uwaye yote uhukumuye, huna udhuru; kwa maana katika hayo umhukumuyo mwingine wajihukumu mwenyewe kuwa na hatia; kwa maana wewe uhukumuye unafanya yale yale. Warumi 2:1 Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha. Warumi 14:4

KWA NINI SHERIA YA MUNGU INAPASWA KUTII?

KWA NINI SHERIA YA MUNGU INAPASWA KUTII? Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. 1 Yohana 3:4 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kama yeye alivyo mtakatifu, kila mwenye matumaini ya kufanana naye, katika yeye hujitakasa. Ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu, na ndivyo tulivyo. Atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; atendaye dhambi ni wa Ibilisi, maana Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kama mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendaye haki amezaliwa na yeye. 1 Yohana 2:29 Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. Yakobo 2:10-11

MTUME ANAITAJE KANISA AMBALO LIMEHARIBIWA NA USHIRIKIANO WA KIDUNIA?

MTUME ANAITAJE KANISA AMBALO LIMEHARIBIWA NA USHIRIKIANO WA KIDUNIA? Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu. Yakobo 4:4 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Ameliita kuwa ni adui wa Mungu, hata laomba, wala halipati kwa sababu laomba vibaya ili livitumie kwa tamaa zake. Nia ya mwili ni mauti, na ni adui juu ya Mungu, hautii sheria za Mungu, wa hauwezi kutii. Kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia, na inapita, pamoja na tamaa zake. Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. 1 Yohana 2:15 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu. Warumi 8:8

JE, MATUKIO NA SIRI ZA MUNGU NI NANI WANAFUNULIWA?

JE, MATUKIO NA SIRI ZA MUNGU NI NANI WANAFUNULIWA? Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake. Amosi 3:7 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Bwana Mungu amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri? Hata Kristo Yesu aliwaita wanafunzi wake rafiki na sio watumwa sababu yote aliyoyasikia kwa Baba yake aliwaarifu. Midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, maana ni mjumbe wa Bwana wa majeshi. Maana mtu mkaidi ni chukizo kwa Bwana, Bali siri yake ni pamoja na wanyofu. Mithali 3:32 Maana, ijapokuwa naihubiri Injili, sina la kujisifia; maana nimewekewa sharti; tena ole wangu nisipoihubiri Injili! 1 Wakorintho 9:16 Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohana; Basi, uyaandike mambo hayo uliyoyaona, nayo yaliyopo, na yale yatakayokuwa baada ya hayo. Ufunuo wa Yohana 1:1,19 Ma...

JE, MUNGU AMEWEKA SIKU YA HUKUMU?

JE, MUNGU AMEWEKA SIKU YA HUKUMU? Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu. Matendo ya Mitume 17:31 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Mungu anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu, maana sisi sote tuu wazao wake. Tumtafute Mungu, ingawa kwa kupapasa-papasa, tukamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu. Akaagiza watu wahubiriwe na kushuhudiwa ya kuwa Kristo Yesu ndiye aliyemuamuru awe Mhukumu wa walio hai na wafu, na kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi. Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki. Mbele za Bwana, kwa maana anakuja, Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa uaminifu wake. Zaburi 96:13 Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa. 1 Petro 4:5

KWA NINI UTEKELEZAJI WA HUKUMU AMEPEWA KRISTO?

KWA NINI UTEKELEZAJI WA HUKUMU AMEPEWA KRISTO? Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake. Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. Yohana 5:26-27 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe, hata kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili tupate kustaajabu. Watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyempeleka. Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu. Matendo ya Mitume 17:31 Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote; Yohana 5:22 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme w...

NI NANI ATAKAYEHUKUMIWA NA WATAKATIFU, NA NI WAKATI GANI?

NI NANI ATAKAYEHUKUMIWA NA WATAKATIFU, NA NI WAKATI GANI? Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? 1 Wakorintho 6:2-3 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Neema na amani zitokazo kwa Yesu Kristo, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia, ametupenda na kutuosha dhambi zetu katika damu yake; ametufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, kwa utukufu na ukuu alio nao milele na milele. Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. Ufunuo wa Yohana 3:21 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu. 1 ...

JE, KUTAKUWA NA UFUFUO WA WAFU WOTE?

JE, KUTAKUWA NA UFUFUO WA WAFU WOTE? Nina tumaini kwa Mungu, ambalo hata hao nao wanalitazamia, ya kwamba kutakuwa na ufufuo wa wafu, wenye haki na wasio haki pia. Matendo ya Mitume 24:15 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Msishangae maneno hayo, maana inakuja saa ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti ya Mwana wa Adamu. Watatoka waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu. Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu, waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele. Danieli 12:2 Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai. Yohana 5:25

WAKATI ATAWAKUSANYA WATEULE WAKE, IKIWA SISI NI MIONGONI MWAO, TUTASIKIA NINI KUTOKA KWA MWOKOZI?

WAKATI ATAWAKUSANYA WATEULE WAKE, IKIWA SISI NI MIONGONI MWAO, TUTASIKIA NINI KUTOKA KWA MWOKOZI? Naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu. Mathayo 24:31 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi. Atawaambia kondoo wake walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; na wale mbuzi walioko mkono wake wa kushoto atawaambia, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake. kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika. 1 Wakorintho 15:52 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na s...

JE, MWOKOZI ATATOKEAJE KWA WALE AMBAO HATIMAYE WANARUHUSIWA KUMWONA?

JE, MWOKOZI ATATOKEAJE KWA WALE AMBAO HATIMAYE WANARUHUSIWA KUMWONA? Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 1 Yohana 3:2 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tukae ndani yake, ili kusudi atakapofunuliwa tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake katika kuja kwake. Mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, hivyo kila atendaye haki amezaliwa na yeye. Kama tu watoto, tu warithi  wa Mungu pamoja na Kristo, tukiteswa pamoja naye ili tupate kutukuzwa pamoja naye. atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake. Wafilipi 3:21 Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu. Wakolosai 3:4 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 1 Yo...

JE,NI NINI PAULO AMBACHO ALISEMA ANAKISUBIRI?

JE, NI NINI PAULO AMBACHO ALISEMA ANAKISUBIRI? baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake. 2 Timotheo 4:8 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Baada ya kuona wakati wake wa kufariki umefika, alisema amevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo ameumaliza, na imani ameilinda. Anachosubiri ni siku ile ya kupewa taji ya haki aliyowekewa, na sio yeye tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake Bwana. Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka. 1 Petro 5:4 Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali. 2 Timotheo 2:5

KRISTO KWENYE KUBADILIKA AKIWAKILISHA UTUKUFU WAKE WA BAADAE, ALIONEKANAJE?

KRISTO KWENYE KUBADILIKA AKIWAKILISHA UTUKUFU WAKE WA BAADAE, ALIONEKANAJE? akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang'aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru. Mathayo 17:2 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Petro, Yakobo na Yohana walipojulisha nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake, hawakufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali walikuwa wameona wenyewe ukuu wake. Alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, walipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu, waliposikia sauti ikitoka mbinguni katika utukufu mkuu "Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye". Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye. Mathayo 17:5

MWOKOZI ATAKUJA KATIKA UTUKUFU GANI?

MWOKOZI ATAKUJA KATIKA UTUKUFU GANI? Kwa sababu kila atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu. Luka 9:26 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Mtu ye yote akitaka kumfuata Kristo Yesu, ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, amfuate. Kila mtu atakayemkiri Kristo mbele ya watu, naye atamkiri mbele za Baba yake aliye mbinguni. Alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu. Marko 8:38 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake....