JE, WATU WAKISHAKUWA WANAFUNZI WA KRISTO, WANATAKIWA KUWA NA NIA GANI? Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; Wafilipi 2:5 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu aliye mbinguni. Ikiwako faraja ya Kristo, ushirika wa Roho wa Mungu, hutuma na rehema, ijalizeni furaha ya Kristo ili mwe na nia moja, mapenzi mamoja, roho moja, mkinia mamoja; wala msitende neno lolote kwa majivuno ila kwa unyenyekevu, na kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe bali pia na aangalie mambo ya wengine. Kristo, mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, na akaona kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho; akajifanya hana utukufu, akatwaa namna ya utumwa , akawa mfano wa mwanadamu, akijinyenyekeza na kuwa na utii hata mauti ya msalaba. Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu; Warumi 12:10 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake. vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo...
KARIBU KWENYE BLOG YENYE TAFAKARI NA MASOMO YA NENO LA MUNGU. MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI; NDIVYO MEMA YATAKAVYOJIA. NENO LAKE ULIWEKE MOYONI MWAKO.