JE, NI MAANDAMANO GANI MAZURI AMBAYO YATAANDAMANA NA KUJA KWA BWANA? Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. 1 Wathesalonike 4:16 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Angalieni, ni siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo. 1 Wathesalonike 4:17-18 Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu. Yohana 17:24
KARIBU KWENYE BLOG YENYE TAFAKARI NA MASOMO YA NENO LA MUNGU. MJUE SANA MUNGU ILI UWE NA AMANI; NDIVYO MEMA YATAKAVYOJIA. NENO LAKE ULIWEKE MOYONI MWAKO.