Skip to main content

Posts

Showing posts from October, 2019

JE, UTAKUJA WAKATI WATU HAWATAISIKILIZA ILE KWELI KWENYE BIBLIA?

JE, UTAKUJA WAKATI WATU HAWATAISIKILIZA ILE KWELI KWENYE BIBLIA? Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. 2 Timotheo 4:3-4 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kweli ipo, ila watu wataikwepa iliyo kweli na kufuata waalimu makundi makundi kwa hadithi na mafundisho ya uongo. Na ukweli upo, ila umepindishwapindishwa na unaendelea kupindishwapindishwa. Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; nawe ujizoeze kupata utauwa. 1 Timotheo 4:1-7 Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu. 2 Wathesalonike 2:15

NI NINI HUSABABISHA WAACHANE NA ZIZI LAO WENYEWE?

NI NINI HUSABABISHA WAACHANE NA ZIZI LAO WENYEWE? Naam, mbwa hao wana choyo sana, hawashibi kamwe; na hao ni wachungaji wasioweza kufahamu neno; wote pia wamegeuka upande, wazifuate njia zao wenyewe, kila mmoja kwa faida yake, toka pande zote. Isaya 56:11 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Hawawezi kufahamu neno sababu wamegeuka upande wakifuata njia zao wenyewe kwa faida zao wenyewe. Wanatimiza mapenzi yao wenyewe badala kutimiza mapenzi ya Mungu. Ni walinzi vipofu wasio na maarifa, hawawezi kulia, huota ndoto, hulala na hupenda usingizi. Kipofu akimuongoza kipofu wanatumbukia shimoni wote wawili. Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya. Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung'aa ya asubuhi. Ufunuo wa Yohana 22:15-16

JE, WANAONYA KUNDI KUHUSU HATARI INAYOKUJA?

JE, WANAONYA KUNDI KUHUSU HATARI INAYOKUJA? Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. 1 Wathesalonike 5:3 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Ndugu, sisi tumekuwa wana wa nuru, wana wa mchana, sisi si wa usiku, wala wa giza hata siku ile itupate kama mwivi. Tujivike vifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu. Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Wameiponya jeraha ya watu wangu kwa juu juu tu, wakisema, Amani, Amani, wala hapana amani. Yeremia 6:14 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina, wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Mathayo 24:38-39

BWANA ANAWAITAJE WACHUNGAJI WA UWONGO, NA WANGAPI WATAWAFUATA?

BWANA ANAWAITAJE WACHUNGAJI WA UWONGO, NA WANGAPI WATAWAFUATA? Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili. Mathayo 15:14 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Jina la Mungu linatukanwa kwa ajili yao, sababu wanayajua mapenzi ya Mungu, wanayakubali yaliyo bora, na wanajua wanaongoza vipofu. Ni wanafiki, maana wanaacha mambo muhimu yawapasayo kufanya, wanawaongoza vipofu kumbe na wao ni vipofu, wanatumbukia wote shimoni. Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia. Mathayo 23:24 Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. 2 Petro 2:2

TUNAWEZAJE KUTOFAUTISHA KATI YA KWELI NA YA UWONGO?

TUNAWEZAJE KUTOFAUTISHA KATI YA KWELI NA YA UWONGO? Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana wa majeshi. Bali ninyi mmegeuka mkaiacha njia; mmewakwaza watu wengi katika sheria; mmeliharibu agano la Lawi, asema Bwana wa majeshi. Malaki 2:7-8 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Yapasa midomo ya kuhani kunena yaliyo maarifa, yaliyo mema  ili watu waifuate sheria kinywani mwake, maana yeye ni mjumbe wa Bwana. Kuhani inapoiacha njia sahihi anawakwaza watu wengi katika sheria. Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi. Isaya 8:20 Sheria ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake; alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha uovu. Malaki 2:6

JE, NI WAKATI GANI SAHIHI KUOMBA MSAADA KWA MUNGU?

JE, NI WAKATI GANI SAHIHI KUOMBA MSAADA KWA MUNGU? Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Wafilipi 4:6 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Wakati wote tumtegemee Mungu katika kila jambo, kwa kuomba na kushukuru. Tumsifu na kumuabudu Mungu Baba siku zote na wakati wote. Maana yeye ndiye yote katika wote. Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani; Wakolosai 4:2 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu. 1 Petro 5:7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu. Wafilipi 4:7

JE, SALA ITAKUWA NA FAIDA GANI KWA MTU ANAYEHUSIKA?

JE, SALA ITAKUWA NA FAIDA GANI KWA MTU ANAYEHUSIKA? Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. Yakobo 1:5 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Mtu akipungukiwa na hekima, aombe kwa Mungu atupaye wote kwa ukarimu, na aombe kwa imani bila shaka yoyote, naye atapewa. Maana mtu mwenye shaka hadhani kama atapokea kitu kwa Bwana. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno. Yakobo 1:4 Ndipo utakapofahamu kumcha Bwana, Na kupata kumjua Mungu. Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu; Mithali 2:5-6

KATIKA KUJENGA TABIA NJEMA, NINI KINGINE NI MUHIMU?

KATIKA KUJENGA TABIA NJEMA, NINI KINGINE NI MUHIMU? Bali ninyi, wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, ya kwamba waliwaambia ya kuwa, Wakati wa mwisho watakuwako watu wenye kudhihaki, wakizifuata tamaa zao wenyewe za upotevu. Watu hao ndio waletao matengano, watu wa dunia hii tu, wasio na Roho. Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu, jilindeni katika upendo wa Mungu, huku mkingojea rehema ya Bwana wetu Yesu Kristo, hata mpate uzima wa milele. Yuda 1:17-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kujijenga katika tabia njema ni kwa kuzidi katika kuomba na kujilinda na upendo wa Mungu kwetu kwa kuyakumbuka na kuyaishi mafundisho yaliyonenwa na mitume wa Kristo Yesu kuwa makini na watu wasio wa Roho , watu wa dunia hii tuu. Basi kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye, wenye kujengwa katika yeye, mmefanywa imar...

JE, NENO LA MUNGU LINAKUWA NINI MOYONI MWAKO?

JE, NENO LA MUNGU LINAKUWA NINI MOYONI MWAKO? Maneno yako yalionekana, nami nikayala; na maneno yako yalikuwa ni furaha kwangu, na shangwe ya moyo wangu; maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi. Yeremia 15:16 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Usirudi nyuma na kuziacha amri zake Mungu, na yatunze maneno yake zaidi ya riziki yako. Maneno yake yakafanye kinywa chako kuwa kitamu kama asali na likiwe furaha na shangwe kwa wengine pia. Akaniambia, Mwanadamu, kula uonacho; kula gombo hili, kisha enenda ukaseme na wana wa Israeli. Ezekieli 3:1 Nikakitwaa kile kitabu kidogo katika mkono wa malaika yule, nikakila; nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu, na nilipokwisha kukila tumbo langu likatiwa uchungu. Wakaniambia, Imekupasa kutoa unabii tena juu ya watu na taifa na lugha na wafalme wengi. Ufunuo wa Yohana 10:10-11

ILI UKUE KWA NENO LA MUNGU, NI LAZIMA MTU AFANYE NINI NALO?

ILI UKUE KWA NENO LA MUNGU, NI LAZIMA MTU AFANYE NINI NALO? Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi. Zaburi 119:11 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Ni lazima Neno la Mungu liwekwe mioyoni mwetu, lihifadhiwe kabisa hapo, ili lituwezeshe kujiepusha na kutenda dhambi. Neno lenye pumzi ya Mungu lafaa sana kwa kufundisha, kuonya, kuongoza na kuadabisha katika haki. Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako. Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako. Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako. Zaburi 119:12,15,16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 2 Timotheo 3:16 Hivyo, tujitahidi sana katika kuwa na muda wa utulivu, moyo wa utulivu na mahali tulivu, ili tupate wakati mzuri na Mungu wa kuzungumza naye kwa kuomba, kushukuru na kusikiliza anasema nini nasi kupitia Neno lake. Maisha ya...

JE, NI NINI KITASABABISHA MKRISTO KUKUA?

JE, NI NINI KITASABABISHA MKRISTO KUKUA? Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu; 1 Petro 2:2 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kwa Mkristo kukua ni kumwendea Kristo Yesu kwa kukaa katika Neno la Mungu siku zote. Na pia kuhakikisha unapata muda wa utulivu, moyo wa utulivu na mahali tulivu na Mungu siku zote. Ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho. Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima. 1 Petro 2:1,4

JE, MTU ANAWEZAJE KUKUA KATIKA NEEMA?

JE, MTU ANAWEZAJE KUKUA KATIKA NEEMA? Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa, na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo. Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo. 2 Petro 1:4-8 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Asiyekuwa na hayo ni kipofu haoni vitu vya mbali na amesahau kutakaswa dhambi zake za zamani, maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe. Tena tusichoke katika kutenda mema, kwa kadri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema. Yeye asemaye kwamba yumo nuru...

JE, MTU HUKAMILIKA WA MAFUNDISHO NA KANUNI ZA KRISTO?

JE, MTU HUKAMILIKA WA MAFUNDISHO NA KANUNI ZA KRISTO? Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu, Waebrania 6:1 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tumekwisha kupewa nuru na kukionja kipawa cha mbinguni na kufanywa washarika wa Roho Mtakatifu na kulionja neno zuri la Mungu na nguvu za zamani zijazo, tuchunge tusianguke, maana twamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zetu. wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri. Waebrania 6:6 Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu; ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili. 1 Petro 2:2-3 Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na ...

JE, MAFUNDISHO YA UKAMILIFU YAMEFUNDISHWA KATIKA BIBLIA?

JE, MAFUNDISHO YA UKAMILIFU YAMEFUNDISHWA KATIKA BIBLIA? Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno. Yakobo 1:4 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tusiogope majaribu, maana kujaribiwa kwa imani huleta saburi, na Neno la Mungu linasemani furaha kuangukia majaribu, na kwa saburi tupate kuwa wakamilifu. Pia, upendo ndio kifungo cha ukamilifu. Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; Yakobo 1:2 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu. Wakolosai 3:14 Hivyo, tusiogope majaribu tukihesabu ni furaha tupu kwa saburi tupate kuwa wakamilifu, na tupendane sisi kwa sisi kama Kristo Yesu alivyotupa amri. Asiyependa hukaa katika mauti. Asiyetenda haki hatokani na Mungu, ni wa ibilisi.

MWENYE MATUMAINI YA KUMUONA MUNGU HUFANYAJE?

MWENYE MATUMAINI YA KUMUONA MUNGU HUFANYAJE? Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 1 Yohana 3:3 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tumeitwa Wana Wa Mungu na ndivyo tulivyo, na ulimwengu haututambui, na itakavyodhihirika, tutafanana naye, maana tutamwona kama alivyo tutakapouvua huu mwili wa kuharibika. Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 1 Yohana 3:1-2 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; 1 Yohana 3:4,7 Hivyo, tutende haki, kama yeye alivyo na haki. Tupendane sisi kwa sisi kama Kristo Yesu alivyotupa...

JE, MTU HUWA NANI ANAPOONGOZWA NA ROHO WA MUNGU?

JE, MTU HUWA NANI ANAPOONGOZWA NA ROHO WA MUNGU? Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; Warumi 8:14,16 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Ukifuata matendo ya mwili unataka kufa, bali unatakiwa kuyafisha mambo ya mwili kwa Roho ili uishi. Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. Wagalatia 5:16

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI?

JE, NI MATENDO GANI YALIYO YA MWILI? Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Wagalatia 5:19-21 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuwe makini hapa, matendo ya mwili sio tuu hayo tuliyoambiwa hapo, ila ni pamoja na yanayofanana na hayo. Kuishi katika Kristo ni kuusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake. Ni kujiepusha na maovu na kujitenga kabisa na matendo mabaya ya mwili. Basi walio katika Kristo waenende kwa Roho, wala hawatatimiza kamwe tamaa za mwili. Mwili hutamani ukishindana na Roho. Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufal...

NI NAMNA GANI HALI YA MTU INAWEZA KUBADILISHWA?

NI NAMNA GANI HALI YA MTU INAWEZA KUBADILISHWA? Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. 2 Wakorintho 5:17 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kuwa ndani ya Kristo ni kulipenda Neno La Mungu, kuliamini na kuliishi. Yote hayo ni kwa kufuata kanuni, amri na maagizo ya Mungu, na yanawezekana tuu kwa kumuamini na kukiri  Kristo alikufa na kufufuka katika wafu na ni Bwana na mwokozi wa maisha yako na kwa kuziacha kabisa maovu. Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Warumi 8:1 Wanaoenenda katika Roho na sio katika mwili.

KIUHALISIA, NI IPI HALI YA WATU WOTE?

KIUHALISIA, NI IPI HALI YA WATU WOTE? kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; Warumi 3:23 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kiuhalisia wote tumekuwa na dhambi, wa si kwa Wayahudi na Wayunani bali kwa wote walio chini ya sheria, chini ya torati. Dhambi huja kwa njia ya sheria, bali haki ya Mungu ipo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa. Warumi 3:24-25 Basi tukiisha kuhesabiwa haki itokayo katika imani, na mwe na amani kwa Mungu, kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, Warumi 5:1

NI LINI MAISHA HAYA YA UZIMA YATAWEKWA?

NI LINI MAISHA HAYA YA UZIMA YATAWEKWA? Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika. 1 Wakorintho 15:51-52 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu.  Sio wote tutalala, lakini wote tutabadilika siku ya parapanda ya mwisho,wafu watafufuliwa kwanza, wasiwe na uharibifu, na walio hai watabadilika. "Miili hii ya kuharibika itavaa kutokuharibika na ya kufa itavaa kutokufa." Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa. 1 Wakorintho 15:53 Hivyo, wapendwa tuimarike, tuzidi kutenda kazi ya Bwana siku zote, maana taabu sio bure katika Bwana.

JE, HUU UZIMA WA MILELE UMEFICHWA VIPI KWA MWAMINI?

JE, HUU UZIMA WA MILELE UMEFICHWA VIPI KWA MWAMINI? Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. Wakolosai 3:3 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Tuvifishe viungo vyetu vilivyo katika nchi, tuepukane na maovu sababu huleta ghadhabu ya Mungu. Yawekeni mbali maovu mkivaa utu mpya. Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima. 1 Yohana 5:11-12 Hivyo, mna uzima wa milele ninyi mnaoliamini jina la Mwana wa Mungu, na  uzima huo umefichwa pamoja naye katika Mungu.

KWA NINI MUNGU ALIMTOA MWANAE MPENDWA AFE? NI NANI PEKEE ANAYEFAIDIKA NA KIFO CHAKE?

KWA NINI MUNGU ALIMTOA MWANAE MPENDWA AFE? NI NANI PEKEE ANAYEFAIDIKA NA KIFO CHAKE? Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia. Yohana 3:16-36 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Mungu aliupenda ulimwengu, ikiwa na maana aliwapenda watu wake wote, na alimtoa Mwanae kwa ajili ya wote. Nia ikiwa ni kila mmoja apate ule uzima wa milele aliotuandalia tokea mwanzo. Agizo ili kuupata uzima huo ni kumwamini Mwana aliyatumwa na yeye. Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. 1 Yohana 4:16 Hivyo, tunakiri Yesu ni Bwana, na twaamini Kristo alikufa na baada ya siku tatu akafufuka katika wafu ili kuupata uzima wa milele. MUNGU ANATUPENDA, ...

UFUFUO WA KRISTO UMEKUWA FAIDA GANI KWETU?

UFUFUO WA KRISTO UMEKUWA FAIDA GANI KWETU? Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. 1 Wakorintho 15:20 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kwa kufufuka Kristo katika wafu, kiyama ya wafu ipo, maana yeye ndiye limbuko lao. Na kama Kristo hakufufuka, imani yetu ni bure. Hivyo waliolala katika Kristo watahuishwa atakapokuja, na hapo ndio mwisho, Kristo atakapompa Mungu Baba ufalme wake. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa. 1 Wakorintho 15:21-22 Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima. Warumi 5:18 Hivyo, tunakiri Yesu ni Bwana, na twaamini Kristo alikufa na baada ya siku tatu akafufuka katika wafu ili kuupata uzima wa milele.

KWA NINI MAUTI HAIKUMSHIKILIA KRISTO KATIKA UTAWALA WAKE?

KWA NINI MAUTI HAIKUMSHIKILIA KRISTO KATIKA UTAWALA WAKE? Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake. 1 Petro 2:22 Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki? Yohana 8:46 Ahimidiwe na atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Yesu hakutenda dhambi kabisa, ndicho kilichomuwezesha kuishinda mauti. Mauti haikuweza kumshikilia kwenye utawala wake yule mwovu. Pamoja na mateso yote, matukano na aibu zote, yeye alijikabidhi kwa Mungu ahukumuye kwa haki. Pamoja na yote hayo, alikuwa na uwezo wa kukataa, na kuuondoa mwenyewe uhai wake na kuutwaa tena. Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake. Isaya 53:7 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki. 1 Petro 2:23 Ndiposa Bab...

KRISTO ANALO JINA ASILOLIJUA MTU.

KRISTO ANALO JINA ASILOLIJUA MTU. Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya. Ufunuo wa Yohana 3:12 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao. Ufunuo wa Yohana 14:1 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kuna jina jipya la Kristo asilolijua mtu, ila litakuwa limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao. Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. 1 Yohana 5:8 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli. Yohana 1:14 Naye ana ...

JE! NI KWA NAMNA GANI TULIPATA UNABII KATIKA MAANDIKO?

JE! NI KWA NAMNA GANI TULIPATA UNABII KATIKA MAANDIKO? Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. 2 Petro 1:21 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Unabii katika maandiko uliwafikia wanadamu kutoka kwa Mungu kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu na si kwa jinsi apendavyo mtu fulani. Neno liliwajia wengine pia kwa Bwana kusema nao katika ndoto. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. 2 Petro 1:20 Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, Bwana, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto. Hesabu 12:6 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa? Hesabu-Numbers 12:8 Hivyo, unabii katika maandiko umewafikia wanadamu kwa baadhi kuong...

JE, NI LINI HIZO AHADI ZA THAMANI ZITAFIKIWA?

JE, NI LINI HIZO AHADI ZA THAMANI ZITAFIKIWA? Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi. Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Waebrania 10:36-38 Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kwa ujasiri tulio nao, tuendelee kuwa na saburi, maana anayekuja hatakawia. Bali tuishi kwa imani bila kusitasita kuokoa roho zetu. Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake. 2 Petro 3:13-14 Hivyo, tuishi kwa imani, tuonekane katika amani bila mawaa, wenye ujasiri, wenye saburi. Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwa...

VITU VINGINE VYA THAMANI ALIVYOAHIDIWA MSHINDI. (2)

VITU VINGINE VYA THAMANI ALIVYOAHIDIWA MSHINDI. (2) Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kwa aliye na sikio asikie maneno haya ambayo Roho anayaambia makanisa. YEYE ASHINDAYE: 1. Atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. Ufunuo wa Yohana 3:5 2. Nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya. Ufunuo wa Yohana 3:12 3. Nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. Ufunuo wa Yohana 3:21 Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao. Yakobo 1:12 Hivyo, tustahimili majaribu ...

VITU VINGINE VYA THAMANI ALIVYOAHIDIWA MSHINDI. (1)

VITU VINGINE VYA THAMANI ALIVYOAHIDIWA MSHINDI. (1) Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na Baba yetu. Kwa aliye na sikio asikie maneno haya Roho ambayo Roho anayaambia makanisa. YEYE ASHINDAYE: 1. Nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. Ufunuo wa Yohana 2:7b 2. Hatapatikana na madhara ya mauti ya pili. Ufunuo wa Yohana 2:11b 3. Nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea. Ufunuo wa Yohana 2:17b 4. Na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, Ufunuo wa Yohana 2:26b Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja. Ufunuo wa Yohana 2:25

NI AHADI GANI KUBWA NA ZA THAMANI ZIMEAHIDIWA WASHINDI?

NI AHADI GANI KUBWA NA ZA THAMANI ZIMEAHIDIWA WASHINDI? Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. 2 Petro 1:4 Ahimidiwe Mungu baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na baba yetu. Kwa kumjua Mungu na Bwana wetu Yesu Kristo tumeahidiwa ahadi kubwa na za thamani. Na mojawapo ya ahadi kuu ni uzima wa milele. Neema na iwe kwenu na amani iongezwe katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu. 2 Petro 1:2 Na hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele. 1 Yohana 2:25 Hivyo, tumjue sana Mungu na kumkiri Yesu ndiye Kristo ili tupate hizo ahadi tulizoahidiwa kama washindi.

NI NANI ANAYETUPA NGUVU YA USHINDI?

NI NANI ANAYETUPA NGUVU YA USHINDI? Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo. 1 Wakorintho 15:57 Ahimidiwe Mungu baba wa Bwana wetu Yesu Kristo na baba yetu, baba wa rehema na faraja yote. Anayetupa ushindi ni Mungu kwa Kristo Yesu,  kwa jinsi anavyotupenda. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Warumi 8:37 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu. Yohana 16:33 Hivyo, tumshukuru Mungu siku zote kwa kutupa ushindi dhidi ya yule adui kwa kupitia Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Tuwe na amani ndani ya Kristo, maana Kristo mwenyewe ameushinda ulimwengu.